Wed, 16 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu, Kocha Msaidizi, Kocha wa Viungo na Kocha wa Magolikipa wa Kitayosce (Tabora United) wote wamekosa vigezo vya kusimama kwenye benchi na wamezuiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana Agosti 15, 2023 na TFF, makocha ambao walisoma chini ya mwaka 2020 walitakiwa kufanya kozi ya maboresho (refresher cource) lakini makocha hao hawakufanya hivyo.
Hivyo, Kitayosce ambayo leo inatarajia kushuka dimbani dhidi ya Azam FC huwenda wakaingia uwanjani bila ya kuw ana kocha hata mmoja.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live