Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Makocha Italia waweka Historia Ligi ya Mabingwa Ulaya

Fbl Eur C1 Psg Real Madrid 2 Makocha Italia waweka Historia Ligi ya Mabingwa Ulaya

Thu, 3 Nov 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ilikuwa hatua nzuri ya makundi kwa makocha wa Italia katika Ligi ya Mabingwa, huku makocha hao wakipeleka timu zao katika hatua ya mtoano ambayo ni 16 bora.

Wawakilishi watatu kati ya wanne wa Serie A katika kinyang’anyiro hicho walitinga hatua ya 16 bora.

Napoli, Milan na Inter zote zitashiriki katika hatua ya mtoano, huku Juventus pekee wakishindwa kutinga hatua inayofuata kufuatia kumaliza nafasi ya tatu katika kundi lake.

Makocha watano wa Italia wamefuzu hadi hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa katika msimu mmoja kwa mara ya kwanza kabisa. Real Madrid ya Carlo Ancelotti, Tottenham ya Antonio Conte, Napoli ya Luciano Spalletti, Milan ya Stefano Pioli na Inter ya Simone Inzaghi zote zitachuana katika hatua ya mtoano.

Massimiliano Allegri atakuwa amechanganyikiwa kutokana na timu yake ya Juventus kushuka kwenye Ligi ya Europa. Sasa wanasubiri kuona ni timu gani watakutana nayo kwenye mechi ya mtoano.

Droo ya hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa itafanyika Jumatatu Novemba 7 saa 11.00 kwa saa za Uingereza.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live