Tue, 14 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Makamu wa Rais wa Yanga, Arafat Ally Haji ambaye pia ni Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Bima la Zanzibar ameshinda tuzo ya Insurance Corporation CEO of the Year 2023.
Tuzo hizo ambazo zinatolewa na jarida la Global Brands la nchini Uingereza, akishinda katika kipengele cha Leadership Awards.
Mbali na Arafat kushinda tuzo hiyo, ameliongoza Shirika la Bima la Zanzibar kushinda tuzo ya Most Reliable Insurance Corporation katika kipengele cha Insurance Awards.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live