Mshambuliaji wa Azam FC, Prince Dube anatarajia kuukosa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Dodoma Jiji utakaopigwa Oktoba 3 kutokana na kusumbuliwa na nyama za paja.
Mshambuliaji wa Azam FC, Prince Dube anatarajia kuukosa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Dodoma Jiji utakaopigwa Oktoba 3 kutokana na kusumbuliwa na nyama za paja. Dube aliiumia kwenye mchezo dhidi ya Singida ambao Azam iliishinda kwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Azam FC, Chamazi. Daktari wa timu hiyo, Dk Mbaruku Mlinga alifunguka kuwa, Dube alipata majeraha kwenye misuli ya paja wamempa mapumziko ya wiki moja baada ya hapo watamfanyia vipimo tena. “Dube atakuwa nje kwa wiki moja na zaidi baada ya hapo atafanyiwa vipimo tena hivyo ni wazi mchezo wa Ligi unaofuata hataweza kucheza.