Mon, 10 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Inaelezwa beki huyo wa kati anahusishwa na kuondoka Manchester United, kama akibaki kikosini hapo anaweza kupoteza cheo hicho ambacho kinaweza kutua kwa Bruno Fernandes.
Uamuzi huo unatarajiwa kufanyika wiki hii kwa kuwa tayari Kocha wa United, Erik Ten Hag ameonesha kutokuwa na mipango ya muda mrefu na Maguire
Maguire alianza katika mechi 8 tu za Premier League msimu uliopita akizidiwa idadi ya mechi na walinzi wenzake wote kikosini hapo; Luke Shaw, Lisandro Martinez, Raphael Varane na Victor Lindelof.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live