Dirisha la usajili limefungwa lakini Klabu zimeendelea na mipango ya kuboresha vikosi kwa madili ya nyota yaliyoshindikana kwenye dirisha lililofungwa hivi juzi.
Real Madrid wamepanga kumsajili mshambuliaji wa Paris Saint-Germain Kylian Mbappé mapema mwezi Januari .
Matajiri hao wa LaLiga wamempa mchezaji huyo kipaumbele pindi dirisha la usajili litakapofunguliwa tena.
Hata hivyo, Plan B ya Madrid endapo watashindwa kufikia makubaliano kamili ya kumsajili watatafuta mbadala wake upande mwingine na hadi sasa machaguo yaliyopo ni washambuliaji wa Manchester City; Erling Haaland na Julian Álvarez.