Mon, 27 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii wa muziki wa Rap nchini, Madee amesema kwa sasa mchezaji wake bora wa Tanzania anacheza mpira soka la kulipwa nchi za nje ni Novatus Dismas anayekipiga katika Klabu ya FC Shakhtar Donetsk nchini Ukraine.
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X zamani Twitter amendika; "Ndio mchezaji wangu bora wakulipwa anayecheza nje ya mipaka ya Tanzania. Tuzo yangu nampa yeye."
Novatus Dismas anacheza nafasi ya beki wa pembeni pia ana uwezo wa kucheza kama kiungo mkabaji na mchezeshaji.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live