Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maddison afunguka kutemwa Uingereza

James Maddison Maddison afunguka kutemwa Uingereza

Thu, 6 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo mshambuliaji wa Tottenham na Timu ya Taifa ya Uingereza James Maddison, ameachwa kwenye kikosi cha wachezaji 26 waliochaguliwa na Kocha wa kikosi hicho Gareth Southgate kwaajili ya Mashindano ya EURO yatakayofanyika Nchini Ujerumani.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alikuwa sehemu ya mchujo wa awali wa wachezaji 33 wa Southgate lakini ameambiwa amekuwa miongoni mwa wachezaji saba waliokatwa kwenye kikosi cha Uingereza. Madison kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ameandika;

"Nilifanya mazoezi vizuri na nilifanya kazi kwa bidii wiki nzima lakini ikiwa ninajiamini, kiwango changu kwa Spurs niliporudi kutoka kwa jeraha katika kipindi cha pili cha msimu huenda hakikuwa katika viwango nilivyokuwa nimeweka jambo ambalo lilimpa Gareth uamuzi wa kufanya.

Bado nilifikiri kungekuwa na nafasi kwa ajili yangu katika kikosi cha wachezaji 26 kwani ninahisi ninaleta kitu tofauti na nimekuwa mhimili mkuu katika kampeni hii nzima ya kufuzu kwa Euro 2024 nchini Ujerumani lakini meneja amefanya uamuzi na sina budi kuheshimu hilo, Nitarudi, sina shaka. Nawatakia wachezaji wenzangu kila la heri huko Ujerumani"

Maddison alicheza mechi ya kirafiki ya England dhidi ya Bosnia-Herzegovina Jumatatu, akitokea benchi katika ushindi wa 3-0 kwenye Uwanja wa St James' Park.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live