Mwamuzi Stéphanie Frappart amechaguliwa na Shirikisho la Soka duniani FIFA kuwa mwamuzi katika mchezo kati ya Costa Rica dhidi ya Ujerumani, ambapo ataweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kuchezesha mechi ya Kombe la Dunia kwa wanaume leo saa 4:00 usiku.
Mwamuzi Stéphanie Frappart amechaguliwa na Shirikisho la Soka duniani FIFA kuwa mwamuzi katika mchezo kati ya Costa Rica dhidi ya Ujerumani, ambapo ataweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kuchezesha mechi ya Kombe la Dunia kwa wanaume leo saa 4:00 usiku. Hata hivyo, haitakuwa mara ya kwanza kwa mwamuzi huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 38 kuandika jina lake katika historia ya soka, kwani pia aliwahi kuwa mwanamke wa kwanza kuwa mwamuzi wa mchezo wa Ligi Kuu Ufaransa Ligue 1 na Ligi ya mabingwa Ulaya UEFA.