Wed, 1 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwekezaji na Rais wa Heshimawa wa Klabu ya Simba SC, Mohammed Dewji 'Mo Dewji' amefanya uteuzi wa wajumbe wanne watakaoingia kwenye Bodi ya Wakurugenzi ya klabu hiyo kuungana na wajumbe wa kuchaguliwa wa upande wa wanachama.
Wajumbe hao ambao Mo amewateua chini ya Mwenyekiti, Salum Abdallah Muhene 'Try Again' ni Dkt. Raphael Chegeni, Hamza Johari, Zulfikar Chandoo na Mhe. Rashid Shangazi.
Hatua hiyo inafuatia kufanyika uchaguzi mkuu uliomrejesha madarakani Mwenyekiti Murtaza Mangungu na Wajumbe Dk. Seif Ramadhan Muba, Asha Baraka, CPA Issa Masoud Iddi, Rodney Chiduo na Seleman Haroub.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live