Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Luis Miquissone Aachwa na Kocha Al Ahly

OFFICIAL Luis Miquissone Joins Al Ahly From Simba SC Luis Miquissone

Fri, 15 Oct 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kocha wa Mabingwa Afrika, Al Ahly, Pitso Mosimane ametaja kikosi chake kitakachosafiri kuelekea Niger kwa ajili ya mchezo wa klabu bingwa dhidi ya USGN.

Katika kikosi hicho Pitso Mosimane amewaacha nyota wawili aliowasajili msimu huu, Luis Miquissone aliyesajiliwa kutoka Simba SC ya Tanzania na Percy Tau aliyesajiliwa kutoka Brighton and Albion ya England.

Kikosi kamili kinachosafiri;

Magolikipa: Lofty, Sobier na Hamza

Mabeki: Rabia, Yasser, Benoun, Ayman, Hany na Maalsoul

Viungo: Akram, Dieng, Hamad, El soulia na Koka

Washambuliaji: Kahraba, Walid, Mohamed Mahmoud, Taher na Sherif.

Imeelezwa kuwa Miquissone na Tau walisajiliwa wakati muda wa kuwasilisha majina ya wachezaji kwa hatua za awali Ligi ya Mabingwa ukiwa umepitwa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live