Kocha wa Mabingwa Afrika, Al Ahly, Pitso Mosimane ametaja kikosi chake kitakachosafiri kuelekea Niger kwa ajili ya mchezo wa klabu bingwa dhidi ya USGN.
Katika kikosi hicho Pitso Mosimane amewaacha nyota wawili aliowasajili msimu huu, Luis Miquissone aliyesajiliwa kutoka Simba SC ya Tanzania na Percy Tau aliyesajiliwa kutoka Brighton and Albion ya England.
Kikosi kamili kinachosafiri;
Magolikipa: Lofty, Sobier na Hamza
Mabeki: Rabia, Yasser, Benoun, Ayman, Hany na Maalsoul
Viungo: Akram, Dieng, Hamad, El soulia na Koka
Washambuliaji: Kahraba, Walid, Mohamed Mahmoud, Taher na Sherif.
Imeelezwa kuwa Miquissone na Tau walisajiliwa wakati muda wa kuwasilisha majina ya wachezaji kwa hatua za awali Ligi ya Mabingwa ukiwa umepitwa.