Thu, 12 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Tottenham Hotspurs haitamuongeza mkataba mshambuliaji wao raia wa Brazil, Lucas Moura na ataondoka klabuni mwishoni mwa msimu huu.
Lucas Moura alijiunga na Tottenham akitokea kwa matajiri wa Ufaransa klabu ya PSG mwaka 2018 huku akisaini mkataba ambao ungemuweka kwa wababe hao wa London mpaka mwaka 2024.
Chini ya Mourinho na Pochettino mshambuliaji huyo alikuwa na wakati mzuri lakini ujio wa Antonio Conte haonekani kuwa na nafasi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live