Tue, 5 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Beki wa Yanga SC, Joyce Lomalisa kuikosa Medeama katika mchezo wa tatu wa hatua ya Makundi ya Klabu Bingwa Afrika utakaopigwa Ijumaa hii, Desemba 8, 2023.
Afisa habari wa kikosi cha Yanga, Ali Kamwe amethibitisha kuwa mlinzi huyo wa kushoto wa kikosi hicho hajasafiri na timu hiyo kutokana na majeraha aliyoyapata kwenye mchezo wa Al Ahly.
Kwenye mchezo huo, Yanga walitoka sare ya 1-1 na hivyo kuwa na alama 1 kwenye msimamo wa kundi lao hivyo kushikilia mkia katika kundi lao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live