Majogoo wa Jiji, Timu ya Liverpool imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ajax katika mchezo wa Kundi A Ligi ya Mabingwa Ulaya jana Uwanja wa Anfield.
Liverpool ambao wana mwendo wa kusua sua tangu kuanza kwa msimu huu ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Mohamed Salah dakika ya 17, kabla ya Mohammed Kudus kuisawazishia Ajax dakika ya 27 na kufanya matokeo kuwa 1-1.
Wakati mchezo ukielekea ukingoni, mlinzi Joel Matip akawahakikishia Liver kuondoka na alama tatu kwa goli la dakika ya 89 lililowapa ushindi Liverpool.
Mchezo huo kati ya Liver na Ajax ulikuwa ni wa hatua ya makundi, kundi A.