Mabingwa mara 6 wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya, Timu ya Liverpool wamepangwa kucheza na Real Madrid katika hatua ya 16 Michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya.
Mechi hiyo ni kumbu kumbu ya Fainali ya msimu uliopita zilizopigwa Jijini Paris nchini Ufaransa ambapo vijana wa Carlo Ancelotti walibeba taji lao la 14 kwa Michuano ya Ulaya baada ya ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Vinicious.
Mechi za hatua ya 16 bora zitapigwa;
Mechi za mkondo wa kwanza zitapigwa katikati ya wiki ya Februari 14/15 na Februari 21/22 mwakani na mechi za marudiano zitakuwa Machi 7/8 na 14/15 mwakani.
Droo ya kupangwa kwa mechi hizo imefanyika mchana wa leo Novemba 7 na mechi nyingine ni kama ifuatavyo;
RB Leipzig vs. Man City
Club Bruges vs. Benfica
Liverpool vs. Real Madrid
Eintracht Frankfurt vs. Napoli
AC Milan vs. Tottenham
Dortmund vs. Chelsea
Inter Milan vs. FC Porto
PSG vs. Bayern Munich