Sun, 19 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabao ya Darwin Nunez dakika ya 10 na Cody Gakpo dakika ya 17 yameipa Liverpool ushindi wa 2-0 dhidi ya Newcastle United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa St. James' Park Jijini Newcastle.
Kwa ushindi huo, Liverpool inafikisha pointi 35 katika mchezo wa 12 na kusogea nafasi ya nane, wakati Newcastle United inabaki na pointi zake 41 za mechi 23 nafasi ya nne.
Liverpool iliyokuwa na matokeo mabovu kwa kipindi kirefu, imefanikiwa kuibuka na ushindi wa pili mfululizo katika michezo migumu ambayo walitarajiwa kukumbana na upinzani mkubwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live