Liverpool imeingia kwenye rekodi ya kushinda michezo saba mfululizo katika Ligi ya Mabingwa kwa vilabu kutoka Uingereza baada ya kuifunga Inter Milan bao 2-0 siku ya Jumatano usiku ikiwa ni hatua ya 16 bora.
Barcelona, Real Madrid na Bayern Munich walikuwa tayari wamefanya hivyo Liverpool wanakuja kwenye hatua hiyo baada ya kushinda michezo yote 6 ya makundi wakimaliza juu kwenye kundi B na kuwa timu ya kwanza ya Premier League kuweka rekodi hiyo.
The Reds ndiyo timu pekee yenye mafanikio zaidi kwenye Ligi ya Mabingwa wakiwa wameshinda ubingwa huo mara sita wakati mataji manne kati ya hayo manne ni wakati michuano hiyo inajulikana kama European Cup (1976-77, 1977-78,1980-81 na 1983-84) na wakati Mashindano yamebadilishwa jina ilikuwa ni mwaka (2004-05, 2018-19).
Liverpool walifuzu kucheza michuano ya Ulaya kwa mara ya kwanza msimu wa 1964-65 na waliweza kufika mpaka nusu fainali ya michuano hiyo.