Mon, 3 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Liverpool imejipanga kuingia kwenye vita dhidi ya Arsenal ili kuipata saini ya kiungo wa Real Madrid, Aurelien Tchouameni dirisha lijalo.
Timu hizi zimeshawishika kutaka kumsajili kiungo huyu kwa sababu hapati nafasi ya kucheza kwenye kikosi cha kwanza cha Madrid kwa msimu huu na amecheza mechi 21 za La Liga.
Mkataba wa fundi huyu unamalizika mwaka 2028 na kiwango kibovu cha Majogoo hao wa Liverpool msimu huu kinaifanya iingie sokoni.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live