Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Lineker: Nawajua wachezaji wawili EPL ambao ni mashoga, watajitokeze!

Gary Lineker Gary Lineker

Mon, 17 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwanasoka wa zamani wa England ambaye kwa sasa ni Mtangazaji wa michezo Gary Lineker (61), amedai kuwa anawajua wachezaji wawili wa Ligi ya England ambao ni mashoga na anatumani kuwa watajitokeza hivi karibuni.

”Huu ndio wakati mwafaka, wakati tunakaribia Kombe la Dunia,mjitokeze mtetee msimamo wenu ”

Akizungumza na gazeti la Daily Mirrow, Lineker alisema “Ninajua kwa uhakika kabisa kuwa hawa watu walikuwa karibu sana kujitokeza, ninawajua ni wapenzi wawili, lakini siwezi kuwataja,”

”Hofu ya Mashabiki na ukosoaji kutoka kwa wachezaji wenzao ndio unawafanya wengi wajifiche, na kubaki wakiishi maisha ya uwongo,”

”Ninajua ni ngumu sana, lakini nilikuwa natamani mjitokeze tu, sababu najua mpo, ni dhahiri kuna wachezaji wengi ambao wanalazimika kuishi kwa uwongo.”

Kombe la Dunia litafanyika mwezi ujao nchini Qatar ambako kutokana na sheria kali za Kiislamu mahusiano ya jinsia moja hayakubaliki na hukumu yake ni kifo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live