Wed, 7 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Manchester United, Erik ten Hag amefanya uamuzi wa kubaki na huduma ya beki wa kati Victor Lindelof baada ya kukoshwa na kiwango chake.
Sasa beki huyo wa kati raia wa Sweden atapewa ofa ya mkataba mpya baada ya kumalizia msimu huu katika kiwango bora kabisa cha ndani ya uwanja.
Mkataba wake wa sasa huko Old Trafford utafika tamati mwakani na Man United imeamua kukifanyia kazi kipengele cha kumwongezea mwaka mmoja zaidi kilichokuwa kimewekwa kwenye mkataba huo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live