Sat, 6 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la Mpira wa miguu nchini TFF, limesogeza mbele tarehe ya kuanza kwa Ligi ya Wanawake maarufu kama Serengeti Lite mpaka Disemba 23 mwaka huu.
Katika taarifa yake TFF, imeeleza kuwa sababu ya kusogezwa mbele ni ushiriki wa Timu ya Taifa ya Wanawake "Twiga Stars" kushiriki katika mashindano ya CECAFA na ile ya U20 kukabiliwa na mchezo wa kufuzu kwa Kombe la Dunia.
Awali Ligi hiyo ilipangwa kuanza Novemba 13.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live