Licha ya kuondolewa kwenye mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC wanazidi kupiga mkwanja tu, unaambiwa mpaka sasa Uwanja wa Azam Complex pale Chamanzi umetumika kwenye mechi 5 kubwa msimu huu nje ya zile za Azam yenyewe.
ASAS FC vs Yanga
Yanga Vs ASAS FC
Yanga vs KMC
Singida FG vs JKU
JKU vs Singida FG
Gharama za kukodisha uwanja wa Chamanzi kwa team za Tanzania kwa mchezo mmoja ni Tsh 5,900,000 (shilingi milioni tano na laki tisa).
Gharama za Kukodisha Uwanja kwa Team za kimataifa ni tsh 12,500,000 , kwa maana hapa sasa ASAS FC ya Djbout wametoa Tsh million 12,500,000 kwa mchezo wao waliochezea nyumbani, JKU si wahapa hapa tu.
Hivyo basi michezo 5 ambazo ziimechezw kwenye Uwanja wa Chamanzi, Azam Fc wamevuna mapato ya Tsh milioni thelathini na sita na laki moja (36,100,000) kwa kipindi kisichozidi wiki tatu tu.