Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Licha ya Kichapo, Pep awapa tano nyota wake

Pep G Meneja wa Man City Pep Guardiola

Wed, 8 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Pep Guardiola amekataa kuwakosa wachezaji wake wa Manchestser City kufuatiwa kupoteza mchezo dhidi ya RB Leipzig kwenye ligi ya mabingwa Ulaya kwa goli 2-1 usiku wa siku ya jumanne.

Dominik Szoboszlai na Andre Silva walikuwa wa kwanza kuifanya RB Leipzig kuongoza kwa goli mbili mbele, kabla ya Riyad Mahrez kuwapatia goli la kufutia machozi kwenye uwanja wa Red Bull Arena, huku mchezo ukimalizika kwa beki wa kulia Kyle Walker kuonyeshwa kadi nyekundu.

“Kipindi cha kwanza tulipoteza umakini na hatukuwa na mawasiliano mazuri, na walikuwa na timu nzuri, lakini kipindi cha pili kilikuwa bora, bahati mbaya tulifanya makosa na walituadhibu, lakini tulicheza vizuri kipindi cha pili.

Tulishambulia sana, tulicheza kushinda mchezo ila tumepoteza hongera kwa Leipzig, tumefanya vizuri kwenye makundi, tumevuka tukiwa tumebakisha mchezo mmoja kwenye kundi gumu, nimeridhika sana na kiwango cha kila mchezo, na natumai mwezi wa pili tutafika tukiwa na hali nzuri.” alisema Pep Guardiola

Chanzo: www.tanzaniaweb.live