Tue, 28 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mlinda Mlango wa Coastal Union raia wa Congo, Ley Matampi ameibuka mshindi wa tuzo ya Golikipa bora na kumpiku mpinzani wake wa karibu Golikipa wa Yanga Djigui Diarra.
Matampi anakwenda kunyakua tuzo ya "Golden Gloves" akiwa na Clean Sheets 15 dhidi ya 14 za Djigui Diarra.
Msimu huu Matampi amekuwa na kiwango bora akiisaidia Castal kumaliza nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu Bara na hivyo kukata tiketi ya kushiriki Michuano ya Kimataifa Msimu ujao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live