Sun, 15 May 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Bayern Munich ya nchini Ujerumani imethibitisha kuwa mshambuliaji wao Robert Lewandowski ameomba kuondoka klabu hapo. Mkurugenzi wa ufundi wa klabu hiyo Hasan Salihamidzic amethibitisha.
Lakini klabu hiyo imemtaka mshambuliaji huyo raia wa Poland mwenye umri wa miaka 33 amalize mkataba wake na The Bavarians unaomalizika Juni 2023.
Msimu huu Lewandowski amefunga mabao 49 katika michezo 45 kwenye mashindano yote.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live