Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Leicester City warejea Ligi Kuu England

Skysports Leicester Promotion 6534628 Leicester City warejea Ligi Kuu England

Sat, 27 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Leicester City imerejea kwenye Ligi Kuu nchini England baada ya Leeds kuchapwa 4-0 na QPR Ijumaa usiku.

Matokeo hayo yanawaacha Foxes kileleni mwa jedwali la ubingwa, kwa pointi nne mbele ya Leeds ambayo inakamata nafasi ya pili.

Leicester City walikuwa wakijifua katika kampeni yao ya kurejea Ligi Kuu mapema msimu huu lakini, baada ya kupotea kwa kiwango kikubwa, wamepata nafuu na kuvuka mstari wa kumaliza.

Jamie Vardy ambaye amedumu katika timu kwa miaka 10 kama mchezaji mwenye kipawa kikubwa akiwa na umri wa miaka 37 amewasaidia kuwarejesha kwenye Ligi Kuu akiwa amefunga mabao 18 katika mashindano yote.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live