Thu, 14 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Kimataifa wa Tanzania, Simon Msuva, juzi alipewa ushindi na Shirikisho la Soka FIFA mbele ya Mabingwa wa Africa Wydad Casablanca akiamriwa kulipwa mishahara na stahiki zake zote na timu hiyo kiasi cha Shilingi za Kitanzania bilioni 1.6
Kwa wakati wote wa kesi yake Msuva hakuwa na timu wala hakueleza hasa nini chanzo cha mgogoro wake na Klabu hiyo ya Morocco.
Sasa leo Julai 14 Msuva anazungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live