Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kwa nini Messi hajawahi kumgusa mwanamke mwingine?

Messi Mkeee Kwa nini Messi hajawahi kumgusa mwanamke mwingine?

Wed, 6 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Unaambiwa Lionel MESSI hajawahi kumgusa mwanamke mwingine zaidi ya mkewe Antonela Roccuzzo aliyeanza naye mahusiano tangu utotoni huko Rosario, Argentina.

Mnamo 2017, Messi na Antonella walifunga ndoa iliyotajwa kama ‘ndoa ya karne’ na kujaaliwa watoto watatu Thiago, Mateo na Ciro.

Raccuzzo ambaye kwa sasa ni Mwanamitindo ana taaluma Udaktari wa meno na mawasiliano ya kijamii aliyosomea katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Rosario kabla ya kujitolea kumsaidia Messi na kuzingatia familia yao.

Kupitia taaluma yake ya Uanamitindo amefanya kazi na chapa maarufu kama Stella McCartney, Adidas, na hivi majuzi, Alo.

Messi anampenda sana mwanamke huyo mrembo amejitolea sana kwake kiasi kwamba hata hawagusi wanawake wengine. Inaelezwa Messi alitaka kuwa mchezaji bora wa soka duniani ili aweze kumhudumia Roccuzzo na kumpa maisha mazuri.

Walipofunga ndoa, mashabiki wengi wa kike walijaribu kujaribu kumshawishi. Shabiki mmoja Suzy Cortez (almaarufu Miss BumBum) alijichora tatoo ya Messi mwilini mwake na kujaribu kumtumia picha zake akiwa katika jezi yake lakini Messi alim-block mara moja.

Messi amekuwa katika muonekano usio wa kawaida anapokuwa karibu na Wanawake wengine katika picha akiibana mikono yake au hata kuiweka mifukoni kuliko kugusana au hata kuweka begani kwa mwanamke mwingine.

Messi hufanya hivyo kuepuka vyombo vya habari kupindisha picha hizo kwa njia isiyo sahihi na kufanya ionekane kuwa kuna kitu kinaendelea wakati hakipo.

Mwanamuziki Shakira alipiga naye picha lakini alijiweka mbali na kuweka wazi kuwa mambo ni ya kiplato kabisa. Hamwekei mikono mwanamke mwingine kwa sababu kwake, ukaribu wa kimwili unabaki kwa mke wake tu.

Messi ni mmoja wa wanaume wachache ambao huweka mipaka kwa wanawake ambao sio mke wake. Anataka kuishi maisha ya faragha na Roccuzzo na watoto wao, na anaweka wazi mara kwa mara kwamba ana upendo wake ni kwa mpenzi wake huyo wa tangu ujanani.

NB: Uhusiano wa kiplato (platonic relationship) ni ule ambao watu wawili wana uhusiano wa karibu lakini hawana uhusiano wa kimapenzi. (Dhana hii inatokana na mawazo ya mwanafalsafa wa kale Plato)

Chanzo: www.tanzaniaweb.live