By Oliver AlbertMore by this Author SIMBA imeanza vizuri hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kushinda mechi mbili mfululizo dhidi ya AS Vita na Al Ahly kwa bao 1-0 kila mmoja.
Timu hiyo inaongoza kundi A ikiwa na pointi sita ikifuatiwa na AS Vita yenye pointi tatu sawa na Al Ahly iliyo nafasi ya tatu huku El Merreikh ya Sudan ikishika mkia ikia haina pointi.
Simba Imepania kufanya makubwa na kutinga robo fainali ya mashindano hayo kama ilivyowahi kufanya hivyo mwaka 2019 huku ikijivunia kikosi bora ilichonacho msimu huu.
2018/ 2019
Ndani ya miaka mitatu ,Simba ilianza safari yake ya mafanikio kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka 2018 kwa kuanzia hatua ya awali kwa kuifunga Mbabane Swallos ya Swaziland mabao 4-1 nyumbani katika mchezo uliofanyika Novemba 28, 2018 kabla ya kuifunga tena ugenini mabao 4-0.