Mon, 2 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Simba wamemiliki sehemu kubwa ya mpira kwenye kipindi cha kwanza kwenye nusu yao ndio maana hawakuweza kuliona lango la Dynamos kwa kiasi kikubwa.
Kipindi cha pili kwa dakika 18, Simba wameweka kambi kwenye nusu ya Power Dynamos na kupeleka mpira zaidi kwenye boksi la Power na unapofanya hivi basi "Chochote" kinaweza kutokea.
Unaweza kupata tuta, ukapata mpira uliokufa karibu na lango au hata bao la kujifunga kama walivyofanya Simba, kilichobaki hapo tena ni kudhibiti mchezo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live