Jana baada ya mechi ya England V/s Italy nilifatilia interview ya kinda wa Real Madrid na England, Jude Bellingham ambaye kwa sasa yupo kwenye kiwango bora sana!
Bellingham anasema watu wengi wanazungumzia kiwango chake kuwa juu kwa sasa, akasema hakuna kitu ambacho kimemuongezea uwezo kama kujiunga na Real Madrid.
Akataja baadhi ya vitu ambavyo vinachochea yeye kuwa katika kiwango bora tangu amejiunga na Real Madrid akitokea Borussia Dortmund.
Ada ya uhamisho, anasema mchezaji akinunuliwa kwa gharama kubwa inakupa deni kichwani. Kila mechi unayocheza sio tu unalazimika kufunga au kutoa assist bali unapaswa kucheza kwa kiwango ambacho kitaisaidia timu kupata ushindi.
Kwa hiyo mchezaji kununuliwa kwa gharama kubwa haikufanyi ubweteke, inakuongezea hamasa na kukupa mzigo mkubwa ambao wengine umewashinda.
Real Madrid ni klabu kubwa yenye wachezaji wenye viwango vikubwa, kwa hiyo kuwa sehemu ya klabu ya aina hiyo inayokukutanisha na wachezaji wakubwa unafanyanao mazoezi, unakutananao dressing room na kuchezanao, inakusaidia kuongeza kiwango chako.