Thu, 29 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Vipers ya nchini Uganda, Roberto Oliviera ameagana rasmi na timu hiyo huku akihusishwa zaidi na Simba SC.
Taarifa kutoka nchini humo zimeeleza kuwa, Kocha ameachana na Klabu hiyo kwa notisi ya muda mfupi na uongozi imekubali kiroho safi na kumtakia kila la heri huko aendako.
Kupitia ukurasa rasmi wa Vipers, wameposti picha yake na kumpongezakwa mafanikio aliyoipa Klabu hiyo na kumtakia kila la heri huku walisema watatangaza benchi mkuu mpya wa benchi la ufundi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live