Kwa mujibu wa Mchambuzi Mkongwe wa Soka nchini Shaffii Dauda ameeleza kwamba winga mpya wa Simba Ladack Chasambi alipata Timu Ulaya ambayo ni Red Bull Salzburg ya nchini Austria lakini haelewi nini kilitokea kiasi cha Chasambi kusaini Simba.
"Niliwasiliana na Ladack Chasambi kumuelekeza juu ya Dili la RB Salzburg ambalo lingefanyika mwenzi huu Januari, akaniunganisha na Meneja wake.
"Meneja wake akaniambia tayari Chasambi ana ofa mbili kutoka Ulaya basi nikafurahi. Baadae nashangaa amesaini Simba. Lakini huwenda Meneja wake ameona ni Dili nzuri ndani ya Simba," amesema Dauda.
Ikumbukwe kuwa, RB Salzburg ndio Klabu anayoitumikia Nyota wa Zamani wa ASEC Mimosas Karim Konate.