Tue, 7 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwamuzi kutoka Tanzania, Heri Sasii, ndiye atakayepuliza kipyenga katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara baina ya watani wa jadi, Simba na Yanga Jumamosi Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Taarifa ya Shirikisho la Mpira wa Miguu TFF hii hapa chini inayoonesha waamuzi na maofisa watakaosimamia mchezo huo.
Waamuzi watakaochezesha mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Simba vs Young Africans na Maofisa watakaosimamia @nbc_tanzania @azamtvtz @tplboard @gsmtanzania @tbc_online pic.twitter.com/NK671mOiNg
— TFF TANZANIA (@Tanfootball) December 6, 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live