Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kovacic kwenye rada za Man City, Bayern

JF SPORT Mateo Kovacic Mateo Kovacic

Thu, 27 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiungo kutoka nchini Criatia Mateo Kovacic amejinasibu kuwa maisha ya klabu ya Chelsea ni kama yupo nyumbani, huku kukiwa na ripoti kwamba analengwa Mabingwa wa England Manchester City na FC Bayern Munich ya Ujerumani.

Kovacic anakaribia miezi 12 ya mwisho ya mkataba wake na Klabu ya Chelsea, na kushindwa kwake kuweka bayana kuhusu mkataba mpya kumesababisha mapendekezo ya kutaka kuondoka.

City wanaweza kuwa sokoni kwa ajili ya kuongezewa safu ya kiungo katika dirisha lijalo la usajili, huku nahodha wa klabu hiyo, Ilkay Gundogan akidaiwa kutathmini ofa ya mkataba kutoka kwa FC Barcelona.

Kovacic pia amekuwa kuungana akihusishwa tena na kocha wa zamani Chelsea, Thomas Tuchel, ambaye amepata mwanzo mgumu wa maisha FC Bayern Munich tangu kuchukua nafasi ya Julian Nagelsmann mwezi uliopita.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 amekuwa chini ya makocha watatu tofauti wakati wa msimu wa misukosuko pale Stamford Bridge, na bado anaridhika kuendelea kukaa hapo Magharibi mwa London.

Akizungumza na vyombo vya habari vya klabu, Kovacic alisema: “Nimekuwa hapa kwa miaka mitano tayari, muda unakwenda, na nimekuwa Chelsea kwa muda mrefu zaidi ya klabu zangu zote.”

“Ninahisi kweli, niko nyumbani. Hakuna kitu cha kutopenda London. Familia yangu inafurahia, ambayo hunirahisishia. Chakula ni sawa, labda si kama Italia au Hispania! Lakini London ni ya kushangaza.”

“Naweza tu kusema mambo mazuri kuhusu London na England. Tunajisikia vizuri sana hapa.”

Kovacic ameanza katika michezo mitatu kati ya minne ya Chelsea tangu Frank Lampard arejee katika klabu hiyo kama Meneja wa muda mapema mwezi huu, ikijumuisha michezo yote miwili ya kushindwa kwa jumla ya 4-0 dhidi ya klabu yake ya zamani ya Real Madrid katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live