Baada ya mazoezi ya wiki mbili, mshambuliaji wa Yanga Hafiz Konkoni yuko tayari kuanza kuonyesha makali yake
Pengine Wananchi watarajie kumuona uwanjani hapo kesho katika mchezo wa fainali Ngao ya Jamii dhidi ya Simba ambao utapigwa uwanja wa Mkwakwani
Konkoni alikuwa mchezaji wa mwisho kusajiliwa na Yanga katika dirisha hili, usajili wake ukikamilishwa siku moja kabla ya dirisha la CAF kufungwa
Konkoni alihitaji angalau wiki mbili za kufanya mazoezi ili kujiweka fiti kabla ya kuanza kucheza mechi za ushindani
Hakutumika katika mchezo wa nusu fanali dhidi ya Azam Fc, lakini matarajio ni makubwa atakuwa na dakika zake kwenye mchezo dhidi ya Simba