Sat, 5 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Afisa habari wa klabu ya Yanga Ali Shaban Kamwe amesema huu ni muda wa kumuacha Gamond kuandaa vitu vyake halafu wakifika Tanga itakuwa ndio muda wa wao kuzungumza kwa miguu yao.
Kamwe amesema kutokea pale atachukua kipaza na kuwaambia kuhusu Maxi Nzengeli mwenye ubora wa Mbappe.
Aidha Ali amesema Skudu Makudubela ni mtu hatari, masta Gamondi anaendelea na vitu vyake pale Avic Town na muda sahihi unakuja na muda sahihi ni pale Tanga.
Yanga itakuwa na mtihani wa kwanza msimu 2023/24 Mkoani Tanga Agosti 9 dhidi ya Azam FC mchezo wa mtoano Ngao ya Jamii.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: