Wed, 20 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Taarifa kutoka Nchini Zambia zimethibitisha kuwa Uongozi wa klabu ya Power Dynamos umemuomba Kocha wa timu ya Taifa ya Zambia Avram Grant Kuongeza nguvu kikosini humo huku wakijiandaa na Mchezo wa marudiano wa CAFCL dhidi ya Simba SC.
Kocha huyo wa Zamani wa Chelsea ya Uingereza Tayari Avram Grant ameanza kazi ya kukinoa kikosi hicho cha Power Dynamos kwa kuwaongezea mbinu vijana hao kuelekea Mchezo wa marudiano dhidi ya Simba utakaochezwa katika dimba la Chamazi.
Mchezo wa awali uliochezwa nchini Zambia uliisha kwa sare ya kufungana magoli 2-2
Chanzo: www.tanzaniaweb.live