Aliyewahi kuwa kocha wa viungo na utimamu wa mwili wa Klabu ya Yanga SC, Riedoh Berdien anatarajiwa kurejea nchini na kujiunga na klabu ya Simba SC.
Atafanya kazi chini ya Kocha mkuu Fadlu Davids ambaye amefikia makubaliano ya kujiunga na Klabu ya Simba SC, kinachosubiriwa ni kutangazwa tu.
Riedoh alifanya kazi na Yanga SC wakati wa bakuli msimu wa 2019|20 na 2020|21. Aliwahi kufanya kazi na Klabu ya Chippa United na Mamelodi Sundowns.
BENCHI JIPYA LA UFUNDI SIMBA;
Fadlu Davids - Kocha mkuu
Darian Wilken - Kocha msaidizi
Mueez Kajee - Mchambuzi wa utendaji
Riedoh Berdien - Kocha wa viungo.
Kocha wa makipa atathibitishwa hivi karibuni kwa sababu Kocha Cadena aliitwa lakini hakuna kilichohitimishwa.