Kocha wa Uganda Cranes, Milutin Sredojevic ‘Micho’ amesema kwamba kuifunga Tanzania sasa imekuwa ndiyo tabia ya Uganda.
Micho ameyasema hayo kwenye mkutano na waandishi wa habari baada ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Taifa Stars kwenye mchezo wa mkondo wa pilj wa kufuzu fainali za CHAN za 2023 na kupata ushindi wa jumla wa 4-0.
"Mwaka 2013 tulipowafunga kwa matokeo ya jumla ya 4-1, wapo waliosema tulibahatisha.
Mwaka 2015 tukawafunga tena kwa matokeo ya jumla ya 4-1, wakasema tena tumewabahatisha.
Lakini ushindi huu wa sasa wa matokeo ya jumla ya 4-0 utamaliza yale maneno ya kwamba huwa tunawabahatisha.
Sasa imekuwa tabia yetu."