Tue, 26 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya mlinzi wa Arsenal Wiliam Saliba kukosekana katika kikosi cha timu ya taifa Ufaransa na watu kuhoji, kocha wa kikosi hicho Didier Deschamps ameibuka na kusema mlinzi huyo ni mchezaji wa kawaida tu.
Kauli hiyo ya Deschamps imezua gumzo kwenye Mitandao ya kijamii baada ya mlinzi huyo kukosekana katika pambano la Ufaransa dhidi ya Ujerumani.
“ Hakuna pengo lolote kukosekana kwa beki huyo ( Saliba). Ni mchezaji wa kawaida “ alisema Deschamps.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live