Mon, 16 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche amesema anahitaji mechi zaidi za kirafiki kukipima kikosi chake lakini pia, haangalii sura ya mchezaji anapopanga kikosi chake.
Kocha huyo ameyasema hayo jana mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Kimataifa wa Kirafiki dhidi ya Sudan na matokeo kuwa sare 1-1.
"Tunahitaji mchezaji wa kuwa tayari kumalizia kule mbele, tunalinda vizuri, tunacheza vizuri katikati lakini nani anakwenda kumalizia kufunga? Tunahitaji wafungaji, mimi siangalii majina mchezaji wa mbele asipofunga nambadilisha," alisema kocha huyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live