Wed, 21 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha mkuu wa timu ya taifa Tanzania ‘ Taifa Stars’ Adel Amrouche ni sehemu ya msafara wa kikosi cha timu ya CR Belouizdad uliokuja nchini kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Yanga , Jumamosi.
Kocha huyo alionekana kuwa karibu na kikosi hicho kuanzia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa (Mw. Nyerere International Airpot) hadi katika kambi ya kikosi hicho katika moja ya Hotel za Kitalii, Jijini Dar es Salaam.
Mwandishi alipomfuata kocha huyo kwa ajili ya kuzungumza nae aligoma na hata mwandishi huyo alimpompiga picha kocha Amrouche alichukua simu ya mwandishi huyo na kuifuta picha yenyewe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live