Mon, 16 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche amesema, anahitaji mechi zaidi za kirafiki ili kuweza kukitengeneza kikosi chake.
Amrouche ametoa kauli hiyo jana mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Kimataifa wa Kirafiki dhidi ya Sudan na kufanikiwa kupata sare ya 1-1.
"Tuna changamoto ya eneno la golikipa, tunahitaji magolikipa ambao watakuwa wanapata nafasi ya kucheza kwenye vilabu vikubwa," alisema Amrouche.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live