Thu, 6 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Tabora Utd imeachana rasmi na kocha Masoud Djuma Irambona na hii ni kutokana na matokeo mabaya wanayopitia Tabora United.
Kwasasa Kikosi cha Tabora Utd kitakuwa chini ya kocha msaidizi Benny Fabian.
Tabora United wanaanza safari leo kuelekea Dar Es Salaam kwa ajili ya mchezo wa marejeano wa Play Off dhidi ya JKT Tanzania.
Mchezo wa kwanza ulimalizika kwa Tabora kukubali kichapo cha mabao 4-0.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live