Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania leo kimesafiri kuelekea nchini Morocco kwaajili ya mchezo wa kwanza wa kutafuta tiketi ya kufuzu fainali za kombe la Dunia 2026 dhidi ya Niger.
Wakati wa maandalizi kocha mkuu wa kikosi cha timu ya Taifa amesema hakutakuwa na uwezekano wa kuwa na timu ya Taifa nzuri kama wachezaji wanaotegemewa wanakaa benchi kwenye klabu zao.
"Kinachosikitisha tuna wachezaji wengi ambao hawachezi kwenye klabu zao. Klabu hazitusaidii, tunaweza vipi kuwa na timu nzuri ya Taifa kama wachezaji wazuri kwenye timu ya Taifa wanakaa benchi".
Upi mtamo wako, anachokisema mwalimu kina uhalisia au ana jitetea kabla ya mambo kuharibika ?.....