Aliyewahi kuwa Kocha Mkuu wa Simba SC na sasa ni kocha wa Amazulu FC ya Afrika Kusini, Pablo Franco Martinez hadi sasa katika michezo ya ligi kuu nchini humo (PSL) amecheza mechi mbili na zote ametoa sare.
Pablo kupitia ukurasa wake wa Instagrama emeonyesha kufurahishwa na namna timu yake imekuwa ikicheza na amesema kwamba anatengeneza timu ya ushindani.
Pablo ameandika; "@pablofrancomartin There are no words to define what these warriors did. Without a doubt we are building something unique. You deserved more and you will get it. Let’s keep going!"
MSIMAMO
Ligi Kuu nchini Afrika Kusini
1. Memelod Sundowns - pointk 6
6. Oralando Pirates - pointi 3
10. Amazullu Fc - pointi 2
11. Chippa United- pointi 2
12.Kaizer Chiefs - pointi 1
16. Cape Town City - pointi 0
Ligi Kuu nchini Afrika Kusini inaonyesha ni ngumu na ina ushindani mkubwa sana. Ukitazama timu kama Cape Town ambayo yupo mkiani hadi sasa, msimu uliopita alimaliza nafasi ya 4 na itashiriki michuano ya kombe la shirikisho CAFCC msimu huu.