Ikiwa inajiandaa kuwavaa wakusanya ushuru wa Manispaa ya Kinondoni KMC jioni ya leo katika dimba la Ali Hassan Mwinyi Mkoani Tabora, Simba SC imechukua tahadhari zote dhidi ya wapinzani wao.
Mchezo huo wa Ligi Kuu NBC, utapigwa majira ya saa 10:00 jioni, lakini Kocha wa Simba Pablo Martin anafahamu fika ubora wa wapinzani wao.
Kocha Pablo anasema;
"Mchezo utakua mgumu sababu KMC wana Kikosi kizuri, na lazima kuwa nao makini. Bado kuna baadhiya wachezaji wetu hawapo vizuri lakini tunaangali nini cha kufanya " amesema Pablo
Simba inahitaji ushindi kwa udi na uvumba ili kupunguza pengo la alama baina yao na vinara wa Ligi Yanga.