Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kocha Mamelodi aukubali mziki wa Yanga

Rulani Mokwena Mchezo.jpeg Kocha Mamelodi aukubali mziki wa Yanga

Sun, 31 Mar 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kocha Mkuu wa Mamelodi Sundowns FC, Rulani Mokwena amesema amekutana na Yanga ngumu ndani ya dakika 90' kama alivyotarajia katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, ingawa imani yake ni kuwa watafuzu hatua ya Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL).

Amesema hayo katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kutamatika mchezo wa hatua ya Robo Fainali ya CAFCL dhidi ya wenyeji Yanga kwa suluhu ya bila kufungana.

"Ninaamini tunaenda kufuzu kwakuwa malengo yetu katika mchezo huu ni kurudi nyumbani tukiwa na hati safi," amesema Mokwena

Mchezo wa mkondo wapili wa hatua ya Robo Fainali utachezwa Aprili 05, 2024 katika Uwanja wa Loftus Versfeld ndani ya Jiji la Pretoria, Afrika Kusini.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live