Wed, 21 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Afrika Kusini Mamelodi Sundowns wametangaa kumuongezea Mkataba kocha wake Rhulani Mokwena mpaka mwisho wa msimu wa mwaka 2026/2027.
Mkataba wa Rhulani Mokwena ulikuwa unamalizika mwishoni mwa mwezi Juni 2023 lakini Kocha huyo hakuonesha nia ya kusaka changamoto mpya.
Mamelodi wameonesha kuridhishwa na mbinu za Kocha huyo pamoja na mafanikio aliyoyapata akiwa na mamelodi msimu wa 2022/23 na hivyo wameamua kumpa Mkataba mpaka mwaka 2027.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live